IQNA

Hassan Nasrullah, shakhsia mwenye ushawishi mkubwa zaidi

12:43 - December 25, 2008
Habari ID: 1722644
Jarida la Newsweek la Marekani limechapisha orodha ya watu wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani na kumuarifisha Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon kuwa ni shakhsia mwenye ushawishi mkubwa zaidi katika ulimwengu wa Kiislamu.
Ripoti ya Newsweek imesema: Nasrullah anapendwa mno na wananchi katika nchi za Kiarabu kwa sababu ya kuushinda utawala ghasibu wa Israel katika vita vya siku 33 mwaka 2006.
Jarida hilo limeandika kuwa wapiganaji wa Hizbullah walilidhalilisha jeshi la Israel katika vita siku 33 huko Lebanon na Sayyid Hassan Nasrullah anatambuliwa kuwa shujaa katika ulimwengu wa Kiarabu.
Jarida la Newsweek ambalo hutoa orodha ya majina ya watu wenye ushawishi mkubwa kila mwaka, limeorodhesha majina ya watu hamsini kama shakhsia wenye ushawishi mkubwa duniani akiwemo Mfalme Abdullah bin Abdulaziz wa Saudi Arabia ambaye limesema: Amepata ushawishi kutokana na nchi yake kuwa na akiba kubwa ya mafuta na taathira zake kwa bei ya mafuta katika masoko ya kimataifa!
338106



captcha