IQNA

Maadili na haki za familia katika Uislamu zajadiliwa

14:19 - February 09, 2009
Habari ID: 1742041
Suala la maadili na haki za familia katika Uislamu limejadiliwa kwa kina katika kongamano la kimataifa la “Kuchunguza sheria za familia katika nchi za Kiislamu” ambalo linafanyika mjini Tehran.
Kongamano hilo linahudhuriwa na wataalamu wa sheria za familia kutoka nchi mbalimbali duniani.
Wataalamu wa kitaifa na kimataifa katika kongamano hilo wamewasilisha makala kuhusu masuala kama vile; ‘uadilifu wa mwanamume na mwanamuke katika Uislamu’, ‘familia na uwezo wa kisheria’, ‘dhamana ya utekelezwaji sheria katika haki za familia katika Uislamu’, ‘kuteswa watoto katika familia’, ‘Watoto wanaolelewa vibaya’ na
‘haki ya mtoto katika nchi za Kiislamu’. 361218
captcha