IQNA

Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani:

Kuzuiwa vazi la hijabu katika leseni ya kuendesha gari huko Minnesota ni ukiukaji wa haki za Waislamu

22:05 - March 05, 2009
Habari ID: 1752147
Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani CAIR limetangaza kwamba muswada uliopendekezwa kwa ajili ya kupiga marufuku vazi za hijabu katika picha za leseni za kuendeshea magari katika jimbo la Minnesota nchini Marekani ni ukiukaji wa haki za kiraia za Waislamu.
Ofisi ya Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani katika jimbo la Minnesota imetangaza kuwa muswada huo unakiuka haki za wafuasi wa dini mbalimbali zinazotumia nembo za kidini.
Muswada huo ambao inasemekana umependekezwa kwa shabaha ya kuimarisha usalama wa taifa, unasisitiza kwamba watu pekee wanaoruhusiwa kuweka picha zenye vazi la hijabu katika leseni za kundeshea magari ni wale wanaolazimika kufanya hivyo kwa sababu za kitiba.
Sheria za sasa za Marekani zinaruhusu kuwa na picha zenye vazi la hijabu katika pasi za kusafiria na vitambulisho mbalimbali.
Siku kadhaa zilizopita uliwasilishwa muswada kama huo huko Oklahoma lakini haukupasishwa kutokana na juhudi za Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani. 373144

captcha