IQNA

Kikao cha "Uislamu na Ukristo: Upendo, Sheria na Demokrasia" kufanyika Scotland

15:39 - August 10, 2010
Habari ID: 1970794
Kikao cha "Uislamu na Ukristo: Upendo, Sheria na Demokrasia" kutafanyika katika siku za tarahe 12 na 13 Agosti katika Chuo Kikuu cha Glascow nchini Scotland.
Katika kikao hicho wataalamu watachunguza uhusiano uliopo kati ya upendo na sheria katika fasihi za dini ya Kiislamu na Kikristo, mazungumzo kati ya dini mbalimbali kwa kutegemea msingi wa upendo na sheria, taathira za nadharia za kidini katika jamii na uhusiano wake na demokasia.
Wahitimu katika taaluma za teolojia, sheria za Kiislamu, elimu jamii, anthropolojia na siasa wanaweza kutuma makala zao katika kikao hicho. 629358



captcha