IQNA

Kongamano la 'Waislamu na Haki za Kiraia' kufanyika Ubelgiji

8:46 - December 09, 2010
Habari ID: 2044833
Kongamano la Waislamu na Haki za Kiraia litafanyika Ijumaa ya tarehe 17 Disemba katika mji wa Brussels nchini Ubelgiji.
Kituo cha habari cha Conference-Islam kimeripoti kuwa kongamano hilo litasimamiwa na Jumuiya ya Kiislamu ya Utamaduni ya Uelgiji (LIIB).
Jumuiya hiyo imewataka watu wote wanaotaka kushiriki kwenye kongamano hilo kuhudhuria vikao vyake kwa ajili ya kuchunguza misingi ya Kiislamu ya kulinda haki za kiraia na sheria zinazohusu haki za wafuasi wa dini mbalimbali.
Wasomi na wanasheria watahutubia kongamano hilo na kujibu maswali ya hadhirina. 709150

captcha