Kanali ya habari ya Rasid imeripoti kuwa maafisa wa Wizara ya Elimu ya Saudia wamemtimua kazi Fauzi Shanar ambaye ni mwalimu katika mkoa wa Qatif kwa tuhuma za kufunza swala kwa mujibu wa mafundisho ya Ahlulbaiti wa Mtume (saw) na kutoa zawadi ya vitabu vya kidini kwa wanafunzi wake.
Tuhuma hizo zilitolewa dhidi ya Fauzi Shanar mwaka uliopita wa masomo na kesi hiyo iliendelea kwa miezi kadhaa hadi jana ambapo Wizara ya Elimu ya Saudi Arabia ilitoa hukumu ya kumuachisha kazi rasmi mwalimu huyo.
Mwalimu huyo mfuasi wa madhehebu ya Kiislamu ya Shia aliyekuwa akifundisha katika shule ya msingi ya Suhaib al Rumi katika mji wa Saihat mkoani Qatif, amewahi kujadiliana na walimu wenzake wa Kiwahabi katika shule hiyo.
Fauzi Shanar ni mwalimu na mwanaharakati wa Kishia ambaye ni maarufu katika eneo anakoishi kwa kuwa na uhusiano mzuri wa kijamii na wakazi wa eneo hilo. 716549