Kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni, viongozi wa jumuiya hizo wanakaribia kupata kibali hicho kutoka kwa wakuu wa televisheni na idhaa ya Uholanzi kuhusu jambo hilo.
Redio ya Kiislamu ya Uholanzi ilifungwa tarehe Mosi Februari na Shirika la Televisheni na Idhaa ya Uholanzi, kutokana na hitilifu zilizozuka kati ya jumuiya hizo za Kiislamu na Akademia ya Kiislamu ya nchi hiyo, jambo lililoungwa mkono na Mhakama ya Amsterdam.
Viongozi wa shirika hilo wamesema kuwa wako tayari kufanya mazungumzo na jumuiya zilizotajwa za Kiislamu kwa madhumuni ya kutatua hitilafu hizo. 745946