Shirika la habari la Interfax limeripoti kuwa Rais Medvedev amewataka wendesha mashtaka, wakaguzi na majaji wa Russia kutoa adhabu kali zaidi kwa watu wanaotenda jinai zinazohusiana na uhasama dhidi ya dini.
Amesisitiza kuwa adhabu kali zinapaswa kutolewa kwa wahalifu ili kuweza kukabiliana na harakati zinazochochea chuki za kidini na kikabila.
Rais wa Russia amesema kutotekelezwa adhabu kali dhidi ya wahalifu ni miongoni mwa sababu za kuongezeka vilitendo vinavyopiga vita dini nchini humo. 748320