IQNA

Ayatullah Qabalan ataka kuimarishwa umoja wa Waislamu na Wakristo Lebanon

13:57 - April 25, 2011
Habari ID: 2111613
Ayatullah Abdul Amir Qabalan, Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu wa madhehebu ya Shia wa Lebanon ametaka kuwepo umoja zaidi kati ya Wakristo na Waislamu wa Lebanon.
Huku akiwapongeza Wakristo wa Lebanon kwa mnasaba wa sikuu ya Pasaka, Ayatullah Qabalan ameelezea matumaini yake kwamba wananchi wa Lebanon watatumia fursa hii ya kidini kwa ajili ya kuimarisha umoja na mshikamano wao. Ameendelea kusema kuwa ni matumaini yake kwamba wananchi wa Lebanon watatumia fursa hiyo kutekeleza vyema majukumu yao ya kidini ambayo yanawataka wote kuishi pamoja kwa amani mbali na mielekeo ya chuki na ubaguzi.
Vilevile amewataka waunde haraka serikali ya umoja wa kitaifa kwa ajili ya kupambana na njama za maadui wao. 780346
captcha