IQNA

Viongozi wa Uzbekistan wazuia kuingizwa nchini humo vitabu vinavyohubiri Ukristo

17:19 - May 11, 2011
Habari ID: 2120427
Viongozi wa Uzbekistan wamezuia kuingia nchini humo vitabu, kanda za video na CD zenye mahubiri ya Kikristo yaliyolenga kuwaathiri vijana wa Kiislamu wa nchi hiyo na kuwaingiza kwenye Ukristo.
Askari usalama wa Uzbekistan pia wamemtia mbarano Anwar Razhabov ambaye alijaribu kuingiza nchini vitu hivyo kinyume cha sheria.
Kwa mujibu wa sheria za Uzbekistan zinazohusiana na masuala ya kidini, hakuna mtu yoyote anayeruhusiwa kuingiza nchini humo vitabu, kanda za video, CD na vitu vingine vinavyokwenda kinyume na mafundisho ya dini zinazotambuliwa rasmi nchini.
Asilimia 92 ya watu wa Uzbekistan ni Waislamu na serikali ndiyo inayohusika na mafunzo ya maimamu na kushughulikia mambo yao katika misikiti tofauti ya nchi hiyo. 789369
captcha