IQNA

Vijana wa Kishia wa mji wa al Awwamiyya walaani kitendo cha kuchomwa Qur'ani Bahrain

15:23 - May 18, 2011
Habari ID: 2124669
Vijana wa Kishia wa mji wa al Awwamiyya nchini Saudi Arabia jana usiku walipiga nara za "Allahu Akbar" na kulaani kitendo cha jeshi la utawala wa Aal Khalifa nchini Bahrain cha kuchoma moto Qur'ani Tukufu.
Wito wa kushiriki katika harakati hiyo ulitolewa katika mtandao wa kijamii wa Facebook. Wito huo uliwataka wakazi wote wa mji huo kutangaza mshikamano wao na Waislamu wenzao wa Bahrain na kulaani vitendo vya kuvunjiwa heshima kitabu kitakatifu cha Qur'ani na kuvunjwa misikiti vinavyofanywa na jeshi la utawala wa Aal Khalifa ukishirikiana na askari kutoka Saudi Arabia. kufuatia wito huo sauti za Allahu Akbar zilisikika jana usiku katika paa za nyumba za mji huo.
Mji wa al Awwamiyya wenye wakazi wengi wa madhehebu ya Shia huko mashariki mwa Saudi Arabia umekuwa ukishuhudia maandamano ya wananchi kwa miezi mitatu sasa ambao wanadai haki zao wa kijamii na kidini.793651

captcha