Uchaguzi huo ulifanyika hapo jana Jumamosi alasiri ikiwa ni moja ya ishara za kuruhusiwa kiwango fulani cha uhuru wa kisiasa na demokrasia tokea wakati wa mapinduzi ya wananchi yaliyofanyika tarehe 25 Januari.
Wamisri waliowengi wamefurahishwa na uchaguzi huo wa kidemokrasia na wa wazi na kuongeza kuwa hayo ni matunda ya mapinduzi ya wananchi waliopigania uhuru wa kujieleza na shughuli za kisiasa.
Maafisa watatu watakaochaguliwa kupitia uchaguzi huo watashughulikia masuala ya uandamizi na utendaji wa harakati ya Ikhwanul Muslimin. 838759