IQNA

Waislamu milioni 3 wa Nigeria waandaliwa futari katika mwezi wa Ramadhani

14:32 - August 14, 2011
Habari ID: 2170219
Mkurugenzi wa shirika la vyakula la Indomie amesema kuwa shirika lake litatoa futari kwa Waislamu milioni tatu wa Nigeria katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Akizungumzia suala hilo, Mr. Temitope Ashiwaju, Mkurugenzi wa Idara ya Uhusiano wa Umma ya shirika hilo amesema kwamba shirika hilo litakuwa likigawa chakula katika misikiti yote muhimu ya nchi hiyo katika mwezi wa Ramadhani. Amesema shirika hilo linazingatia sana umuhimu wa kuimarisha mawasiliano na wateja wake na kwamba mwezi wa Ramadhani umeliandalia fursa nzuri ya kuweza kushirikiana zaidi na wateja hao.
Kwa mujibu wa shirika hilo Baraza la Maimamu la Nigeria limeunga mkono mpango wa shirika hilo wa kutoa futari kwa Waislamu na kwamba wakuu wa misikiti ndio watakasimamia shughuli ya kugawa futari katika misikiti hiyo.842199
captcha