IQNA

Kikao cha kigezo cha Qur'ani katika mwamko wa Kiislamu chafanyika Tehran

12:54 - August 19, 2011
Habari ID: 2173374
Kikao cha Kigezo cha Qur'ani katika Mwamko wa Kiislamu kimefanyika pambizoni mwa Maonyesho ya 19 Kimataifa ya Qur'ani yanayoendelea mjini Tehran.
Kikao hicho ambacho kilifanyika jana jioni kimehutubiwa na mkuu wa Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu la Iran Muhammad Baqir Khurramshad. Kikao hicho kimehudhuriwa na wadau wa masuala ya Qur'ani, wasomi na watafiti wa sayansi ya Qur'ani.
Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur'ani yaliyoanza tarehe 28 Julai hapa mjini Tehran yataendelea hadi 26 Agosti. 845923

captcha