Limesema kuwa mbali na vituo vya usalama, afya na huduma za dharura kwa ajili ya wafanyaziara, idara zote za mji huo zitafungwa kwa ajili ya kuheshimu siku hiyo ya maombolezo kutokana na kifo cha mtukufu huyo wa Nyumba ya Mtume (saw).
Mkuu wa idara ya upashaji habari ya baraza hilo amesema kwamba kwa mujibu wa maamuzi ya baraza hilo, idara zote zinazosimamia masuala ya ulinzi, afya na usalama pamoja na huduma kwa ajili ya wafanyaziara zitatakiwa kuendesha shughuli zao kama kawaida katika siku hiyo ya maombolezo. 846129