Ibrahim Abdul Aziz Sahad amesema kuwa Walibya wanataka kuundwa serikali ya kidemokrasia, inayoheshimu utawala wa sheria na sheria za Kiislamu.
Amesisitiza kuwa serikali yoyote itakayotawala Libya na kudai kuwa inaheshimu haki na uhuru wa wananchi inapaswa kutilia maanani kwamba Walibya ni Waislamu.
Katibu MKuu wa Harakati ya Uokovu wa Libya amesema kuwa wasiwasi wa baadhi ya nchi za Magharibi juu ya kuwepo wanamgambo wa Kiislamu au kwamba wanaharakati wa Kiislamu wanadhibiti hali ya Libya hauna maana yoyote. 854038