IQNA

Askafu wa Wamaroni wa Lebanon asisitiza juu ya kusambazwa fikra za Imam Musa Sadr

15:21 - September 18, 2011
Habari ID: 2189122
Beshara Boutros ar- Rai, Askofu Mkuu wa Wakristo wa Kimaroni wa Lebanon ametaka kusambazwa kwa fikra za Imam Musa Sadr aliyetekwa nyara na utawala wa dikteta wa Libya Kanali Muammar Gaddafi.
Askafu huyo amesisitiza kwamba amekuwa akifanya juhudi za kueneza fikra za msomi huyo wa Lebanon kadiri ya uwezo wake.
Askofu ar-Rai amewata wananchi wote wa Lebanon kurejea historia yao ya kuishi pamoja kwa amani Waislamu na Wakristo wa nchi hiyo na kuimarisha hali hiyo katika siku zijazo. Amesema Wakristo na Waislamu wa Lebanon wana jukumu moja nalo ni la kuishi pamoja kwa amani hatika kila hali. Amesema mji wa Ba'labak ambao aliutembelea hivi karibuni ni nembo na mfano bora wa kuishi pamoja kwa amani makundi mawili ya Wakristo na Waislamu nchini Lebanon. 862719
captcha