IQNA

Serikali ya Niger yaruhusu kusailiwa mwana wa Gaddafi

10:57 - October 02, 2011
Habari ID: 2197082
Waziri wa Sheria wa Niger ametangaza kuwa Baraza la Taifa la Mpito la Libya linaweza kumsaili Saadi Gaddafi, mwana wa kiume wa dikteta mtoro wa Libya aliyekimbilia nchini himo.
Maro Amadou amesema, maafisa wa Baraza la Taifa la Mpito la Libya ambalo limetambuliwa rasmi na serikali ya Niamey wanaweza kwenda Niger na kumsaili Saadi Gaddafi.
Ameongeza kuwa suala hilo halina maana kwamba serikali ya Niger itamkabidhi Saadi Gaddafi kwa viongozi wa Libya.
Saadi Gaddafi alikimbilia nchini Niger baada ya kusambaratika serikali ya baba yake Muammar Gaddafi ambaye hajulikani aliko. 871275
captcha