IQNA

Elfu tatu wamekamatwa London kwa tuhuma za kuhusika katika machafuko

22:15 - October 08, 2011
Habari ID: 2201099
Watu elfu tatu wamekamatwa na polisi ya London, Uingereza kwa tuhuma za kushiriki katika machafuko ya mwezi Agosti mjini humo.
Afisa mmoja wa polisi ya Uingereza ambaye aliongoza operesheni ya kutiwa nguvuni watu hao amesema kuwa, operesheni hiyo ilikuwa kama mashindano ya mbio za nyika.
Christopher Greny amesema kuwa timu kubwa ya askari iliundwa kwa ajili ya kuwakamata watu walioshiriki katika machafuko ya mwezi Agosti mjini London na kuzuia yasienee katika miji mingine.
Ameongeza kuwa picha za video zimetumika kuwatia nguvuni watu walioshiriki katika machafuko hayo.
Awali Scotland Yard ilitangaza kuwa watu 2952 walitiwa nguvuni katika machafuko hayo. 875720


captcha