IQNA

Umoja wa Mataifa wataka kufanyika uchunguzi huru kuhusu mauaji ya Maspero

15:26 - October 12, 2011
Habari ID: 2203862
Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imewataka viongozi wa Misri kufanya uchunguzi huru na usiopendelea upande wowote kuhusu matukio ya eneo la Maspero mjini Cairo yaliyopelekea kuua na kujeruhiwa makumi ya waandamanaji.
Msemaji wa Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa amelitaka pia jeshi la Misri kuwalinda raia wote wa Misri wakiwemo wafuasi wa dini za waliowachache.
Rupert Colville amesema kuwa kamisheni hiyo inawataka viongozi wa Misri wachukue msimamo huru na usiopendelea upande wowote katika uchunguzi wa matukio ya Maspero.
Ripoti nyingine zinasema kuwa Baraza la Makanisa ya Mashariki ya Kati limetoa taarifa likilaani machafuko na ghasia za Misri na limewataka viongozi wa nchi hiyo kuchukua hatua kali za kurejesha amani na utulivu nchini himo.
Watu 24 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa katika ghasia za Jumapili iliyopita katika eneo la Maspero mjini Cairo zilizohusisha Wakristo wa Kikopti na askari usalama. 878370
captcha