IQNA

Ban Ki-moon ataka kukomeshwa mzingiro wa Gaza

18:40 - October 19, 2011
Habari ID: 2208250
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha zoezi la ubadilishanaji mateka kati ya Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Taarifa iliyotolewa na Ban Ki Moon imeeleza kwamba Ban Ki-moon anakaribisha makubaliano yaliyofikiwa na kusema kwamba ana matumaini kuwa mzingiro wa Gaza utamalizika hivi karibuni.
Katibu Mkuu wa UN amesema kuwa kubadilishana mateka kati ya Hamas na Israel ni hatua muhimu katika njia ya kurejesha amani Mashariki ya Kati.
Amesema anatajia kwamba Israel itachukua hatua mpya za kukomesha mzingiro wa Gaza na kulijenga upya eneo hilo.
Amezipongeza pia nchi za Misri na Ujerumani ambazo zimechangia katika kufikiwa makubaliano hayo ya kubadilishana mateka. 883320
captcha