IQNA

Kikao cha kwanza cha kesi ya Televisheni ya Nasma kufanyika Novemba

13:35 - October 23, 2011
Habari ID: 2210087
Kikao cha kwanza cha kusikiliza kesi inayoikabili Televisheni ya Nasma ya Tunisia kimepangwa kufanyika mwezi ujao wa Novemba.
Televisheni hiyo ilifunguliwa mashtaka baada ya kurusha hewani filamu ya Persepolis inayovunjia heshima matukufu ya Kiislamu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Mashtaka hayo yaliwasilishwa mahakamani na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Tunisia, mawakili 144 na raia kadhaa wa nchi hiyo.
Hata hivyo Mwendesha Mashtaka Mkuu wa serikali ya Tunisia amekataa ombi la chama kimoja cha siasa nchini humo ambacho kilikuwa kimetaka kufungwa matangazo ya Televisheni ya Nasma hadi baada ya uchaguzi wa leo wa Baraza la Waasisi.
Baada ya televisheni hiyo kurusha hewani filamu ya katuni inayoonyesha picha iliyodaiwa kuwa ni ya Mwenyezi Mungu, Waislamu wa Tunisia walifanya maandamano makubwa wakipinga kitendo hicho kinachovunjia heshima matukufu ya Kiislamu. 885175

captcha