IQNA

Al Maliki:

Mabaki ya utawala wa Saddam wanataka kuigawa Iraq

10:31 - October 31, 2011
Habari ID: 2214871
Waziri Mkuu wa Iraq Nouri al Maliki amesema kuwa mpango wa kuanzisha mfumo wa federali katika mkoa wa Salahuddin una lengo la kuigawa Iraq.
Al Maliki amesema kuwa mkoa huo umekuwa maficho ya amani kwa mabaki ya utawala ulioondolewa madarakani wa Kibaath na magaidi.
Waziri Mkuu wa Iran amesema kuwa mfumo wa utawala wa federali ni suala la kisheria lakini kutangazwa kadhia hiyo sambamba na kutoa tuhuma dhidi ya serikali na kuzungumzia hitilafu za kimadhehebu na chama cha Baath ni jambo linalotia shaka kubwa.
Nouri al Maliki ameutaja mkoa wa Salahuddin kuwa ni sawa na moto unaotokota chini ya majivu na kuongeza kuwa wafuasi wa dikteta wa zamani wa Iraq wanataka kuufanya mkoa huo kuwa makimbilio ya amani kwa makundi ya kigaidi. 889932
captcha