Ayatullah Issa Qasim aliyasema hayo jana katika hotuba za Swala ya Ijumaa mjini Manama na akawataka Wabahrain kutotumbukia katika moto wa fitina za kimadhehebu.
Amesema kuwa watu wanaochochea moto wa fitina za kimadhehebu wanataka kuwasha moto wa pande zote kwa ajili ya kuutumia vibaya na kudhibiti hali ya mambo kwa maslahi yao. Amesisitiza kuwa maisha na mali ya wananchi haina thamani yote kwa watu wa aina hii.
Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Manama ameuambia utawala wa kifalme wa Bahrain kwamba ni jinai kubwa ya kisiasa kuzusha fitina za kimadhehebu kati ya wananchi.
Vilevile amewahimiza Waislamu wa madhehebu za Shia na Suni kujiepusha na fitina hizo.
893248