Awali mashindano hayo yalipangwa kuanza ijumaa iliyopita ya tarehe 13. Taasisi iliyotajwa imesema kuwa sababu ya kuakhirishwa mashindano hayo ni kuwa washiriki wake wengi walikuwa kwenye mapumziko ya muhula wa kwanza wa masomo. Imesema wengi wa washiriki wa mashindano hayo ni wanafunzi.
Sehemu ya mwisho ya mashindano hayo itaanza tarehe 4 Februari na kuendelea kwa muda wa siku 10.
Ahmad Swafar as-Suweidi, mwanachama wa kamati inayoandaa mashindano hayo amesema kuna washindani 264 wanaoshiriki katika hatua ya mwanzo ya mashindano hayo ambapo washindi watapewa fursa ya kushiriki katika hatua ya mwisho. 935439