Mpango huu unatumia teknolojia ya kisasa na wafanyakazi wenye ujuzi wa hali ya juu ili kuinua kwa kiwango kikubwa ubora wa huduma na ufanisi wa kiutendaji, kuhakikisha waumini na wageni wanapata huduma zote kwa urahisi usio na kifani na kwa kufuata kikamilifu taratibu zilizowekwa.
Mamlaka hiyo imezidi kutumia teknolojia ya kisasa na zana za kidijitali kuwahudumia waumini wa Umrah na wauamini wengine wote wanaofika katika misikiti hiyo ikiwa ni mkakati wa pamoja unaoendana na zama za kidijitali, ukisaidiwa na ujuzi, uwezo, na utendaji bora wa wafanyakazi na washirika wa mamlaka hiyo.
Lengo kuu ni kuwawezesha waumini kupata huduma zote kwa urahisi na kwa mtiririko mzuri, huku wakizingatia kanuni na taratibu za kiutawala.
Mamlaka hiyo imezindua huduma nane za kidijitali kwa ajili ya wageni, zikiwemo huduma za kuweka miadi na kuboresha uzoefu wa ibada.
Miongoni mwa huduma hizo pia ni huduma ya usafiri wa pamoja katika misikiti miwili mitakatifu. Kila mwaka, mamilioni ya mahujaji kutoka kila pembe ya dunia hufika katika misikiti miwili mitakatifu wakati wa msimu wa Hija na Umrah.
3494656