Mashindano hayo yatafanyika katika awamu tano za watoto wenye umri wa miaka 5-8, miaka 9-13, miaka 14-18 na vijana wenye umri wa zaidi ya miaka 18. Vilevile kutakuwepo mashindano ya hifdhi ya juzuu ya kwanza ya Qur’ani Tukufu.
Lengo la mashindano hayo limetajwa kuwa ni kunyanyua juu uwezo wa kisoma Qur’ani kati ya washiriki. Viwango vya washindani vitatathminiwa na majaji wa mashindano hayo kwa kuzingatia kanuni za tajwidi, makharij ya herufi na kadhalika.
Kila mshiriki katika mashindano hayo atapewa dakika tatu za kusoma sehemu ya sura ya Qur’ani itakayochaguliwa na majaji.
Tarehe ya kufanyika mashindano ya utangulizi itatangazwa baadaye na Darul Qur’an wal Itra na washindi wa mashindano hayo ya mwanzo watapata fursa ya kushiriki kwenye awamu ya mwisho ya mashindano hayo. 950099