IQNA

Warsha ya Qur'ani yafanyika Pakistan

17:57 - May 21, 2012
Habari ID: 2330996
Warsha ya mafunzo ya Qur'ani Tukufu iliyoandaliwa na Chuo cha Qur'ani cha New Garden Town imefanyika katika chuo hicho kilichoko katika mji wa Lahore nchini Pakistan.
Warsha hiyo imewashirikisha maelfu ya wanafunzi ambao wamejadili na kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali ya Qur'ani. Arif Rashid, mtaalamu mashuhuri wa masuala ya Qur'ani nchini Pakistan amefundisha na kutoa hotuba kuhusu kitabu hicho kitakatifu katika warsha hiyo ya siku moja. Chuo cha New Garden Town hutoa huduma mbalimbali zinazohusiana na Qur'ani zikiwemo za masomo ya Qur'ani kwa wale wanaovutiwa na masomo hayo. 1012619
captcha