IQNA

Kongamano la 'Qur'ani na Ahlul Beit (as)' lafanyika Pakistan

18:03 - May 27, 2012
Habari ID: 2335372
Kongamano la 'Qur'ani na Ahlul Beit (as) lilifanyika jana Jumamosi huko katika mji wa kihistoria wa Multan katika jimbo la Punjab nchini Pakistan kwa udhamini wa Majlisi ya Umoja wa Waislamu wa Pakistan.
Kongamano hilo limehudhuriwa na wanazuoni, wasomi, wanafikra na shakhsia mashuhuri wa Kishia na Kisuni kutoka pembe zote za Pakistan. Lengo la kongamano hilo limetajwa kuwa ni kuwaunganisha Waislamu wa madhehebu za Kiislamu. Katika kongamano hilo Hujjatul Islam wal Muslimin Nassir Abbas Jaffar Katibu wa Majlisi ya Umoja wa Waislamu wa Pakistan na pia Muhammd Amin Shahidi naibu katibu wa majlisi hiyo walitoa hutuba na kuzungumzia malengo ya kuandaliwa kongamano hilo pamoja na ratiba zake. Wamesema kongamano hilo limeandaliwa kwa madhumuni ya kuimarisha mwamko na umoja wa Kiislau miongoni mwa Wapakistan. 1017514
captcha