IQNA

Mwanamke wa kwanza wa Saudi Arabia kushiriki mashindano ya kimataifa ya Qur'ani

18:04 - June 09, 2012
Habari ID: 2342926
Wanawake wa Saudi Arabia watashiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu ambayo yamepangwa kufanyika hivi karibuni nchini Jordan.
Kwa mujibu wa gazeti la Arab News, Hassanat Bint Ali al-Hureithi ambaye ni mwanafunzi katika Jumuiya ya Hifdhi ya Qur'ani Tukufu mjini Madina anatazamiwa kuiwakilisha Saudi Arabia katika mashindano hayo. Akizungumzia suala hilo, Mansur al-Masih, Katibu Mkuu wa Sekritarieti ya Mashindano ya Qur'ani katika Wizara ya Masuala ya Kiislamu ya Saudi Arabia amesema wizara hiyo imechukua uamuzi wa kumtuma binti huyo kwenye mashindano hayo baada ya kupokea mwaliko kutoka kwa Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Jordan. Amesena kushiriki kwa mwanamke huyo wa Saudia katika mashindano hayo kutawapa wanawake wengine wa nchi hiyo moyo na hamu zaidi ya kujihusisha na masuala ya Qur'ani. 1024298
captcha