Mashindano hayo ambayo yatawashirikisha vijana walio na umri wa chini ya miaka 25 yatafanyika kwa usimamizi wa Rais Abdul Aziz Bouteflika wa nchi hiyo.
Waziri wa Masuala ya Dini na Wakfu wa nchi hiyo ametoa taarifa akisema kuwa mashindano hayo ambayo yatafanyika mwishoni mwa mwezi mtukufu wa Ramadhani hufanyika kila mwaka na kwa usimamizi wa rais wa nchi hiyo. Washindi wa mashindano hayo hutunukiwa zawadi katika siku za sherehe ya Idul Fitr ambapo viongozi wa serikali na mabalozi wa nchi za Kiislamui pamoja na wanazuoni wa nchi hiyo hushiriki.
Waziri huyo ameongeza kuwa kuna mipango mingine ya kuandaa mashindano ya kimataifa kama hayo kwa vijana walio na umri wa chini ya miaka 15. 1030628