IQNA

Hania:

Kujiuzulu Barak ni matokeo ya kushindwa Israel Ukanda wa Gaza

16:49 - November 27, 2012
Habari ID: 2454689
Waziri Mkuu wa serikali halali ya Palestina amesema kuwa kujiuzulu siasa Waziri wa Vita wa utawala haramu wa Israel ni matokeo ya kipigo kikubwa na kushindwa Israel katika vita vya siku nane vya Gaza.
Ismail Hania ambaye alikuwa akitembelea taasisi za vyombo vya habari zilizoharibiwa katika mashambulizi ya Israel kwenye Ukanda wa Gaza amesema kuwa kujiuzulu siasa Waziri wa Vita wa Israel kunaonesha kuwa wavamizi wa Kizayuni wamepata kipigo kikubwa na kushindwa vibaya katika mshambulizi yao ya Gaza.
Ni vyema kuashiria hapa kuwa kushindwa jeshi la utawala wa Kizayuni katika mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Ukanda wa Gaza, kumemlazimisha Waziri wa Vita wa utawala huo atangaza kujiuzulu siasa.
Kwa mujibu wa duru za habari za utawala wa Kizayuni wa Israel, Ehud Barak ametangaza kwamba anajiuzulu siasa na hatogombea tena uchaguzi wa Bunge wa tarehe 22 Januari.
Kujiuluzu huko kwa Waziri wa Vita wa Israel kumetangazwa katika hali ambayo katika siku kadhaa zilizopita Barack alitishia kwamba mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Gaza yatafanywa kwa muda mrefu.
Kufuatia hatua hiyo Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imesema kwamba kujiuzulu Waziri wa Vita wa Israel kumetokana na ushindi wa muqawamah wa Palestina. Fauz Barhum msemaji wa Hamas amesema kwamba, kujiuzulu Ehud Barack Waziri wa Vita wa Israel kunaonyesha kuwa utawala wa Kizayuni haukufanikisha hata lengo moja kati ya malengo yake ya kisiasa na kijeshi katika mashambulizi yake ya hivi karibuni dhidi ya Ukanda wa Gaza. Ameongeza kuwa, hatua hiyo inaonyesha kushindwa Israel na kushinda mapambano ya Palestina. 1143820
captcha