IQNA

Mafunzo ya sayansi ya Qur'ani yapigwa marufuku Ethiopia

18:00 - December 29, 2012
Habari ID: 2472051
Serikali ya Ethiopia imepiga marufuku masomo ya aina yoyote ya tafsiri ya Qur'ani na sayansi ya kitabu hicho kitukufu katika ofisi za Kituo cha Utamduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Addis Ababa.
Maeneo mbalimbali ya Ethiopia yamekumbwa na maandamano ya mara kwa mara tangu baada ya kuanza wimbi la mwamko wa Kiislamu katika nchi za kaskazini mwa Afrika.
Ili kuzuia wimbi hilo, serikali ya Ethiopia imeweka vizuizi vingi ikiwa ni pamoja na mipaka ya kufanyika mahfali za kidini na vikao vya kiraa ya Qur'ani nchini humo.
Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Adis Ababa pia kimelazimika kusimaisha darsa za tafsiri ya Qur'ani na sayansi ya kitabu hicho kutokana na mashinikizo ya serikali ya Ethiopia. 1162175
captcha