IQNA

Mohsen Haji-Hassani Kargar

Maqarii waendeleze malengo ya Qur'ani Tukufu

8:09 - June 15, 2015
Habari ID: 3314406
Mwakilishi wa Iran katika Mashindano ya 57 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Malaysia amesema maqarii au wasomaji wa Qur'ani Tukufu ni wahubiri wa Uislamu na wanapaswa kuendeleza malengo ya Qur'ani.

Akizungumza na IQNA baada ya kuibuka mshindi katika kitengo cha qiraa, Mohsen Haji-Hassani Kargar amesema lengo lake katika mashindano si kupata nafasi ya kwanza bali ni kusonga mbele katika njia ya Qur'ani Tukufu.
Amesema ameridhika ni kisomo chake na ameelezea matumaini yake kuwa washiriki wa mashindano hayo wataendeleza utamaduni wa Qur'ani katika nchi zao.  Haji Hassani Kargar ameyataja mashindano ya Qur'ani kuwa ni fursa kwa Waislamu kuelekea katika utekelezaji mafundisho ya Qur'ani na pia kuimarisha umoja wa Waislamu duniani../mh

3313986

Habari zinazohusiana
captcha