IQNA

Kinara wa Daesh (ISIS) ajeruhiwa nchini Iraq

16:23 - October 12, 2015
Habari ID: 3384677
Kinara wa kundi la kigaidi la Daesh au ISIS, Abubakar al-Baghdadi amejeruhiwa katika hujuma ya Jeshi la Anga la Iraq..

Jeshi la Iraq limesema kuwa, kikosi chake cha anga kimeshambulia msafara wa al-Baghdadi ambaye pia anajulikana kwa jina la Ibrahim al-Samarrai, katika mkoa wa Anbar ulioko magharibi mwa nchi hiyo.
Hata hivyo taarifa ya jeshi hilo imesema, hatima ya kiongozi huyo wa Daesh haijulikani na kwamba kwa sasa anauguza majeraha katika sehemu isiyojulikana.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, mapema leo kundi hilo la kitakfiri limewaangamiza wanachama wao 60 baada ya kuwashuku kuwa wanataka kuliasi kundi hilo.
Al-Baghdadi ambaye alijitangaza kuwa mkuu wa kundi la hilo la Daesh mwaka jana, alijeruhiwa katika shambulizi la anga la Marekani mwezi Machi mwaka huu.

3384300

Kishikizo: isis baghdadi iraq jeshi
captcha