Kwa mujibu wa taarifa marhhoum Sheikh Asfour ambaye alikuwa qarii maarufu katika radio nchini humo alizikwa Ijumaa katika mji waZefta jimboni Gharbia.
Mwendazke alizaliwa mwaka 1938 katika kijiji la Mit al-Rakha, jimbo la Gharbia, kaskazini mwa Misri na alianza kusoma Qur’ani Tukufu akiwa mototo mdogo na alifanikiwa kuhifadhi Qur’ani Tukufu kikamilifu akiwa na umri wa miaka 9.
Alijifunza Tajweed na Qiraa ya Qur’ani Tukufu kutoka kwa Sheikh Mustafa Mahmoud al-Anosui. Akiwa nna umri wa miaka 13 alipokea cheti cha Tajweed kutoka kwa Sheikh Anousi.
Alianza kusoma Qur’ani katika misikiti na hafla mbali mbali na baada ya muda usio mrefu umashuhuri wake ulivuma kote Misri.
Harakati za Qur’ani Misri zimeifanya nchi hiyo iwe na wasomaji bora zaidi wa Qur’ani katika ulimwenguni.