IQNA

Al Azhar yasisitiza kuwa chanjo ya COVID-19 haibatilishi Saumu ya Ramadhani

15:00 - April 07, 2021
Habari ID: 3473791
TEHRAN (IQNA)- Kituo cha Kiislamu ya Al Azhar kwa mara nyingine imesisitiza kuhusu Fatwa yake ya awali kuwa kudungwa chanjo ya COVID-19 au corona hakubatilishi Saumu ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Katika taarifa Jumanne, Idara ya Fatwa za Kwa njia ya Intaneti katika Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar imesema Waislamu wanaweza kudungwa chanjo ya COVID-19 wakiwa wamefunga Saumu katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Taarifa hiyo imesema chanjo zote cha COVID-19 zinalenga kuimarisha mfumo wa kinga mwilini na hazitazamwi kama chakula au kinywaji.

Pamoja na hyo Al Azhar imependekeza kuwa, ikiwezekana, wanaolenga kudungwa chanjo ya COVID-19 wafanya hivyo baada ya Futari kwa sababu yamkini baadhi ya wenye kudungwa chanjo ya Corona wakahitajia lishe ya haraka  au wakalazimika kumeza dawa kutokana na athari za chanjo hiyo.

3962886

captcha