IQNA

Ibada ya Hija yagubikwa na COVID-19

16:14 - July 20, 2021
Habari ID: 3474115
TEHRAN (IQNA)- Ibada tukufu ya Hija ilianza rasmi jana chini ya usimamizi na sheria kali za kukabiliana na maambukizo ya virusi vya Corona huku idadi ya Mahujaji ikiwa chache mno kutokana na vizingiti vilivyowekwa na utawala wa Saudia.

Ni Waislamu 60 elfu tu wenye umri wa miaka 18-65 ndio wanaoshiriki katika ibada ya Hija mwaka huu na wote wamechanjwa na kisha kupimwa tena COVID-19.

Saudi Arabia imewapiga marufuku  Waislamu kutoka nje ya nchi kwa mwaka wa pili mfululizo kutekeleza ibada ya Hija. 

 
 
captcha