Hayo yamedokezwa na Hujjatul Islam wal Muslimin Muhammad Hussein Rafiei ambaye ameongeza kuwa mashindano hayo hulenga kuimarisha ufahamu wa Qur'ani Tukufu na Hadithi miongoni mwa wanachuo, waliohitimu na familia zao.
Hujjatul Islam wal Muslimin Rafiei ambaye pia ni mkuu wa Idara ya Qur'ani na Hadithi katiika chuo hicho amesema mashindanyo yam waka huu ambayo ni ya 27 yanamalizika Jumatano na kwamba washiriki wameshindana katika kategoria 27. Amesema miongoni mwa kategoria zilizokuwepo ni mashidano ya kuhifadhi na kusoma Qur'ani Tukufu, Adhana, Ibtihal na Qaswida.
Amesema mashindano hayo yalijumuisha washiriki 14,000 wanaofungamana na chuo hicho na kuongeza kuwa, mashindano pia yamefanyika katika matawi ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al Mustafa katika nchi kama vile Afghanistan, Iraq, Uturuki, Russia, Turkmenistan, Indonesia, Thailand, Sri Lanka, Bangladesh, Madagascar, Niger, Nigeria, Tanzania na Pakistan.