IQNA

Qur'ani Tukufu

Mitazamo mitano ya Uislamu kuhusu umaskini

18:01 - May 24, 2022
Habari ID: 3475291
TEHRAN (IQNA) - Wakati fulani swali linazuka kuhusu namna Uislamu unavyoutazama umaskini na utajiri ni upi kwa mujibu wa aya za Qur'ani Tukufu na ni kipi chenye kuwa wa thamani. Lakini kwa kusoma vitabu vya Kiislamu inabainika wazi kwamba jibu la swali hili si rahisi sana.

Lakini kwa kusoma vitabu vya Kiislamu inabainika wazi kwamba jibu la swali hili si rahisi sana.

Wakati tunaporejea katika vitabu Kiislamu, ni wazi kwamba haiwezekani kuwasilisha ufahamu wa pamoja kuhusu "umaskini", "utajiri", "utajiri", nk.

Ikiwa tunataka kufahamu kwa kifupi mtazamo wa maandiko ya Kiislamu kuhusu nukta hizo misamiati hiyo tuliyoitaja ambayo inasemekana kuwa nia ya kiuchumi, basi kuna nukta tano zifuatazo ambazo zinaibuka.

1.Wakati umaskini unasifiwa.

 Mtume Muhammad SAW anasema ,“Ufukara ni fahari; najivunia umaskini." Pia inasemekana kwamba Siku ya Kiyama, masikini watakuwa kundi la kwanza kuingia Peponi.

2. Makabiliano hasi na umasikini.

"كَادَ الْفَقْرُ أَنْ يَكُونَ كُفْراً" "Umasikini unaweza kuwa kufru". Ikiwa tunataka kuwa na tafsiri fasaha ya maneno haya, tunaweza kusema kwamba "inakaribia tusema kuwa, umaskini hauna maana nyingine isipokuwa kufru au kutoamini."

3. Pia kuna maelezo kuhusu utajiri na unavyotukuzwa kama njia ya kustawisha familia.

4.Aidha kuna maandiko ya Kiislamu yanayokataza utajiri kama aya hii ya 34 ya Surat Tawba:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ كَثِيرًا مِنَ الْأَحْبَارِ وَالرُّهْبَانِ لَيَأْكُلُونَ أَمْوَالَ النَّاسِ بِالْبَاطِلِ وَيَصُدُّونَ عَنْ سَبِيلِ اللَّهِ ۗ وَالَّذِينَ يَكْنِزُونَ الذَّهَبَ وَالْفِضَّةَ وَلَا يُنْفِقُونَهَا فِي سَبِيلِ اللَّهِ فَبَشِّرْهُمْ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

"Enyi mlio amini! Hakika wengi katika makuhani na wamonaki wanakula mali za watu kwa baat'ili na wanazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu. Na wanao kusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie khabari ya adhabu iliyo chungu."

5. Kunayo maandiko mengine ya Kiislamu kuhusu "Kafaf" na nukta hii haijazingatiwa sana. Utoshelevu kwa hakika ni hali baina ya umaskini na utajiri, ambayo kwayo mwanadamu haongezi au kupunguza. Mtu hutumia kadiri anavyopata; Hali hii imesifiwa sana na inasemekana waja maalumu wa Mungu wako katika hali hii.

* Marejeo: Maelezo ya Seyed Mohammad Hadi Gerami, mhadhidi  wa Kitivo cha Taasisi ya Insia na Mafunzo ya Utamaduni kuhusu fikra za kiuchumi katika Uislamu

4055336

captcha