IQNA

Watoto kadhaa Washiriki Usomaji Wa Qur'ani Tukufu Karbala Arbaeen Mwaka 2023

11:44 - September 07, 2023
Habari ID: 3477563
KARBALA (IQNA) - Watoto kadhaa wa Kiislamu kutoka nchi mbalimbali wanaonyesha ujuzi wao wa Qur'ani Tukufu walipokuwa wakishiriki katika maandamano ya mwaka huu ya Arbaeen.

Sherehe ya maombolezo ya Arbaeen inasimama kama kutaniko la ajabu na kubwa la kidini katika kiwango cha kimataifa, na zaidi ya Wafanyaziyara milioni 20 wanahudhuria. Tukio hili kubwa linaashiria siku ya 40 baada ya Ashura, ukumbusho adhimu wa kuuawa shahidi Imam Hussein (AS), mjukuu  wa Mtume Muhammad (SAW).

Kila mwaka, mkusanyiko mkubwa wa waumini wa Kishia hukusanyika juu ya Karbala, nyumbani kwa madhabahu takatifu ya Imam Hussein (AS), kushiriki katika ibada za maombolezo zenye umuhimu mkubwa. Wfanyaziyara hawa, wengi wao wakitokea Iraki na Irani, hufunga safari ngumu, wakipitia masafa marefu kwa miguu.

Arbaeen ya mwaka huu inakuja huku kukiwa na wimbi jipya la vitendo vya uvunjifu wa heshima wa Qur'ani Tukufu  ambavyo vinaruhusiwa kutokea katika mataifa ya Nordic, hasa nchini Sweden na Denmark, chini ya kivuli cha uhuru wa kujieleza.

 

3485052

 

 

captcha