TEHRAN (IQNA) – Moja ya sifa za Qur’ani Tukufu ni kuwa mshauri. Ni Kitabu kinachotusaidia kuishi maisha bora na kamwe hakitudanganyi.

Huenda kuna watu ambao tunakabili maishani wanaojifanya kuwa wenye huruma lakini kisha wakatudanganya na kutupotosha. Lakini Qur'ani Tukufu haiko hivyo. Ni mshauri mwenye huruma na busara ya kweli.
Imam Ali (AS), katika Nahj al-Balagha, anasisitiza sifa hii ya Qur'ani Tukufu.
Anasema katika Khutba ya 176 ya Nahj al-Balagha: “Wa Astansihu ala Anfusakum (Tafuteni ushauri wake kwa ajili yenu wenyewe).”
Mtu anaweza kuuliza kuhusu neno Anfusakum na kwa nini ni wingi. Ni kwa sababu Nafsi yetu (nafsi) ina viwango vitatu:
Kwa mujibu wa maelezo ya Ibn Maytham Bahrani kuhusu Nahj al-Balagha, maana ya Imam Ali (AS) kwa kuiita Qur'ani Tukufu Nasih (mshauri) ni kutoa nasaha dhidi ya Nafs al-Ammarah, akisema kwamba wakati Nafs al-Ammarah inamhimiza mtu kutenda dhambi, Qur'ani Tukufu inatutakia kheri na inatuonya dhidi ya kufuata matamanio ya dunia.