
Huenda kuna watu ambao tunakabili maishani wanaojifanya kuwa wenye huruma lakini kisha wakatudanganya na kutupotosha. Lakini Qur'ani Tukufu haiko hivyo. Ni mshauri mwenye huruma na busara ya kweli.
Imam Ali (AS), katika Nahj al-Balagha, anasisitiza sifa hii ya Qur'ani Tukufu.
Anasema katika Khutba ya 176 ya Nahj al-Balagha: “Wa Astansihu ala Anfusakum (Tafuteni ushauri wake kwa ajili yenu wenyewe).”
Mtu anaweza kuuliza kuhusu neno Anfusakum na kwa nini ni wingi. Ni kwa sababu Nafsi yetu (nafsi) ina viwango vitatu:
- Nafs al-Ammarah. Ammarah maana yake ni kuhimiza kutenda mabaya. Nafsi hii inatuchochea kuelekea katika dhambi na kwa sababu kufanya madhambi ni kinyume na hekima, Nafsi hii haifuati akili. Nafs al-Ammarah ndio hali ya chini kabisa ya Nafs na katika Hadithi, tunashauriwa kukabiliana nayo ili isiweze kutwaa nafsi zetu..
- Nafs al-Lawamah. Lawamah maana yake ni majuto na lawama. Mtu anapokosea au kutenda kosa, mara moja hujuta na kujikemea. Hii inatokana na Nafs al-Lawamah. Jina la Nafsi hii linatokana na Aya ya 2 ya Sura Al-Qyiamah: “Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
- Nafs al-Muthmainnah. Ni hali ya juu kabisa ya Nafs. Ina maana kwamba mtu amefikia hali ya yakini na amani ya kiroho kutokana na kufuata akili na kuepuka dhambi kwamba kutotenda dhambi ni kawaida yake. Mwenyezi Mungu anasema katika Aya ya 27-30 ya Surah Al-Fajr: “Ewe nafsi iliyo tua! Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. Basi ingia miongoni mwa waja wangu, Na ingia katika Pepo yangu.”
Kwa mujibu wa maelezo ya Ibn Maytham Bahrani kuhusu Nahj al-Balagha, maana ya Imam Ali (AS) kwa kuiita Qur'ani Tukufu Nasih (mshauri) ni kutoa nasaha dhidi ya Nafs al-Ammarah, akisema kwamba wakati Nafs al-Ammarah inamhimiza mtu kutenda dhambi, Qur'ani Tukufu inatutakia kheri na inatuonya dhidi ya kufuata matamanio ya dunia.