IQNA

Waziri wa mambo ya ndani wa Iraq asisitiza uhakikisho wa usalama wakati wa sherehe za nusu  Shaaban huko Karbala

17:27 - February 04, 2025
Habari ID: 3480159
IQNA – Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iraq amesisitiza maandalizi ya kukidhi mahitaji ya usalama katika mji wa Karbala wakati wa sherehe za nusu  Shaaban.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari akiwa na gavana wa Karbala na makamanda wa usalama, Abdul Amir al-Shammari alisema kuwa mpango maalum wa kiusalama na huduma kwa ajili ya kuhakikisha usalama umejadiliwa kwa kina na serikali ya Karbala pamoja na viongozi wa usalama.

Alieleza kuwa mpango huo umepitiwa kwa undani na mahitaji yote ya vikosi vya usalama kwa ajili ya kulinda usalama wa mahujaji yamekamilishwa.

Awali, Nasif al-Khattabi, Gavana wa Karbala, alitangaza kuwa mipango ya huduma, afya, na usalama imeandaliwa kwa ajili ya sherehe hizo.

 Alisema kuwa hakuna vizuizi vya barabara, hali ya usafiri inaendelea vizuri, na juhudi za kiintelijensia na kiusalama ziko katika kiwango cha juu.

Sikukuu ya Nisfu Shaaban, inayoadhimisha kuzaliwa kwa Imam Zaman (Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake), huadhimishwa tarehe 15 ya mwezi wa Hijria wa Shaaban.

 Waislamu wa madhehebu ya Shia kote duniani huadhimisha tukio hili lenye baraka mnamo Februari 14 mwaka huu.

 

 

3491731

 

 

captcha