IQNA – Qari kijana wa Iran Mohammad Hossein Azimi alivutia hadhirina kwa usomaji wa kurasa za 193-194 za Surah al-Balad na aya za mwisho za Surah Al-Fajr wakati wa 'Mahafali ya Kushikamana na Kujikurubisha na Qur’ani.'
Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Husainiya ya Imam Khomeini jijini Tehran mnamo Machi 2, 2025 mbele ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei, pamoja na baadhi ya maqari mashuhuri wa Iran.