IQNA

Mwanamke mwenye hijabu Ufaransa ashambuliwa

9:10 - November 03, 2013
Habari ID: 1309362
Kundi la watu wanaopiga vita Uislamu nchini Ufaransa limemshambulia mwanamke mmoja Muislamu aliyekuwa na vazi la hijabu na kumjeruhi vibaya.

Kituo cha Ajib kimeripoti kuwa, mwanamke huyo alishambuliwa akiwa pamoja na watoto wake wanne kwenye duka moja kubwa katika mji wa Troyes.

Watu hao waliomshambulia awali walivunjia heshima na kutusi dini tukufu ya Uislamu na kisha wakampiga mwanamke huyo wakitaka kumvua vazi lake la hijabu.

Maafisa wa dula hilo kubwa walioshuhudia tukio hilo walimsaidia mwanamke huyo Muislamu na kumtoa mikononi mwa wahalifu.

Mwanamke huyo amewasilisha malalamiko polisi ambayo tayari imeanza uchunguzi.

Mwanamke huyo amepewa likizo ya mapumziko kutokana na majeruhi yaliyosababishwa na shambulizi hilo. 1310070

captcha