IQNA

Spika wa Bunge la Italia asema Uislamu ni dini ya amani

11:33 - October 19, 2014
Habari ID: 1461624
Spika wa Bunge la Italia amesema kuwa, dini ya Kiislamu haipaswi kufungamanishwa na vitendo vya kufurutu mipaka vinavyofanywa na makundi ya kitakfiri na kigaidi kama vile Daesh na kusisitiza kwamba jamii ya kimataifa inapaswa kuelewa kwamba misingi ya dini ya Kiislamu ni kutangaza amani na upendo na inalaani ghasia na machafuko

Akizungumza  kwenye kongamano  lililoandaliwa na Jumuiya ya Waislamu kwenye Msikiti Mkuu wa Rome  lenye mada 'Ugaidi hapana, Uislamu dini ya amani', Spika Laura Boldrini amesisitiza kwamba kundi la kigaidi la Daesh siyo tishio pekee kwa nchi za Magharibi bali ni tishio pia kwa ulimwengu mzima na hasa kwa Waislamu. Spika wa Bunge la Italia amesema kuwa, wananchi wa Italia wanaamini kwamba, Uislamu siyo ule unaozungumzwa na kutekelezwa na magaidi wa Daesh, bali Uislamu ni dini ya amani na upendo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Daesh ni moja kati ya makundi makuu ya kigaidi ambayo yanapata uungaji mkono wa kifedha na kisilaha na nchi za Magharibi  na hasa Marekani, Uingereza na Ufaransa wakisaidiwa na watawala wa  nchi za Kiarabu kama vile Saudi Arabia na Qatar kwa lengo la kuleta ghasia na machafuko na hatimaye kuziangusha serikali halali za Syria na Iraq.../mh

1461192

Kishikizo: uislamu AMANI ugaidi daesh
captcha