IQNA

Wiki ya kuufahamu Uislamu yaandaliwa Birmingham Uingereza

12:05 - November 09, 2008
Habari ID: 1706131
Wiki ya kuufahamu Uislamu itafanyika katika mji wa Birmingham Uingereza kuanzia tarehe 18-27 Novemba kwa ushirikiano wa baraza la mji huo katika maktaba kuu ya mji huo.
Kwa mujibu wa ukurasa wa intaneti wa gazeti la Birmingham Mail , walioandaa programu hiyo wamesema, lengo ni kuuarifisha Uislamu halisi ili kukabiliana na propaganda chafu na zisizo za kweli ambazo zimekuwa zikienezwa dhidi ya jamii ya Waislamu. Kwa mujibu wa Alan Rudge Mkuu wa Baraza la Mji wa Birmingham aliyetangaza rasmi wiki hiyo ya kuufahamu Uislamu, programu hiyo itajumuisha maonyesho ya filamu, mihadhara na usomaji mashairi. Ameongeza kuwa, kuandaliwa wiki hiyo kutakuwa fursa nzuri ya mazungumzo huru na ya kweli.
Itakumbukwa kuwa zaidi ya asilimia 2.7 (Millioni 1.6) ya watu milioni 60 wa Uingereza wanajitambulisha rasmi kama Waislamu. 317128
captcha