Junaid bin Adrus ambaye alikuwa akizungumza na mwandishi wa IQNA amepongeza maamuzi sahihi ya majaji wa Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Wanafuzi wa Vyuo Vikuu mjini Tehran na akasema, utendaji wa kamati ya majaji wa mashindano hayo umeridhisha mno.
Msomaji huyo wa Quran kutoka Misri amesema, hii ni mara yake ya kwanza kuhudhuria mashindano ya kimataifa ya wanafunzi wa vyuo vikuu na kwamba ameshangazwa mno na jinsi viongozi na wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanavyozingatia na kutoa umuhimu mkubwa kwa Qur’ani Tukufu.
Kuhusu kupata kwake nafasi ya tatu katika mashindano ya kusoma Qur’ani, Bin Adrus amesema, uhodari wa wasomaji mashuhuri wa Kimisri kama Ahmad Nuaina na Abul Einein Sheisha ndiyo sababu ya mafanikio ya wasomaji Qur’ani wa Kimisri na kwamba wawakilishi wa Misri wamekuwa wakipata nafasi za juu katika mashindano ya kimataifa ya Qur’ani Tukufu.
Duru ya pili ya Mashindano ya Kimataifa ya Qura’ani ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu yalimalizika jana mjini Tehran . 320050