IQNA

Kikao cha mazungumzo kati ya Uislamu na Magharibi kufanyika Oxford

14:37 - November 17, 2008
Habari ID: 1709301
Kikao cha mazungumzo kati ya Uislamu na Magharibi kinatazamiwa kufanyika hivi karibuni katika Kituo cha Utafiti wa Kiislamu cha Oxford nchini Uingereza.
Mwandishi wa IQNA amesema, wasomi na wanazuoni kutoka nchi mbalimbali duniani watajadili na kubadilishana mawazo kuhusu suala la mazungumzo kati ya Uislamu na Magharibi katika kikao hicho. Gazeti la al Khalij la Umoja wa Falme za Kiarabu limeripoti kuwa Mshauri wa Masuala ya Kidini na Kisheria wa serikali ya Imarati Ali al Hashimi atawakilisha nchi hiyo katika kikao hicho.
Ali al Hashimi ameashiria ujenzi wa msikiti wa Sheikh Zayid katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Oxford na akasema, ujenzi wa msikiti huo umo katika awamu zake za mwisho. 321194
captcha