Kuhusiana na suala hilo, serikali ya Iraq imewataka wananchi wasiegeze magari yao katika barabara kuu za miji hiyo na karibu na maeneo ya kidini na masoko ili kuzuia uwezekano wa kutokea milipuko ya kigaidi katika maeneo hayo. Wakati huohuo, askari usalama wa Iraq wametoa taarifa wakiwataka Wairaqi wote kushirikiana nao katika kudhamini usalama na kuzuia kutokea kwa vitendo vya ugaidi katika siku hii muhimu. Taarifa hiyo imewataka polisi pia kuchukua hatua za ziada za usalama na kutumia kila mbinu ili kuzuia vitendo vya utumiaji nguvu na ugaidi katika maeneo nyeti ya nchi hiyo. 331476